Ndoa Siyo Doa na Mchg. Charles K. Mbogoma
Mchungaji Charles Kuya Mbogoma anahudumu katika Vision of Grace Centre (VGGC) iko jijini Dar es Salaam.
Kitabu hiki cha "Ndoa Siyo Doa" ni matokeo ya kipindi nilichokuwa nakiendesha katika televisheni ya Sibuka, miaka 2012 na 2014; kipindi kilichoitwa "Ndoa Siyo Doa" ambacho nilikianzisha kwa malengo ya kutoa ushauri naishi ili jamii inayopitia kwenye changamoto zinazoumiza katika ndoa, ipate kuhudumiwa; hii ni pamoja na jinsi ya kuzitatua changamoto hizo mbalimbali zinazohusu ndoa, kwa hekima, busara na maarifa kwa kumtegemea Mungu.
Dondoo zifuatazo zimo katika kitabu hiki:
- Dondoo 48 Unazotakiwa Kuzijua Kuhusu Ndoa ya Upendo,
- Ndoa Ni Umoja na ni Taasisi ya Kutusafisha Njia,
- Ndoa Haiji Kukutia 'Doa' bali kukutoa kwenye Doa la Dhambi,
- Hatuchekani Ila Tunajengana Kupitia Madhaifu Yetu Kwenye Ndoa.
| Seller | PASTORKUYABOOKS |
|---|---|
| Author | Mchg. Charles K. Mbogoma |
| Good Read | No |
| Total Pages | 78 |
| Publisher | - |